Sunday, 29 May 2016

Why Educated Women Are More Likely to Be (Happily) Married


According to a Stephanie Coontz op-ed piece in the New York Times, for a woman seeking a satisfying relationship, there has never been a better time to be highly educated.
Men in the 1950s were threatened by the thought of a woman with more or even as much education as they had. But over the past 30 years, these prejudices have changed. “The sociologist Christine B. Whelan reports that by 2008, men’s interest in a woman’s education and intelligence had risen to No. 4, just after mutual attraction, dependable character and emotional stability.”
“Certainly, some guys are still threatened by a woman’s achievements,” the article continues. “But scaring these types off might be a good thing. The men most likely to feel emotional and physical distress when their wives have a higher status or income tend to be those who are more invested in their identity as breadwinners than as partners and who define success in materialistic ways. Both these traits are associated with lower marital quality.”
So if you’re a smart, strong, successful woman, what does this mean for you? Coontz breaks it down like, well, a certain dating coach for smart, strong, successful women:
“For a century, women have binged on romance novels that encouraged them to associate intimidation with infatuation; it’s no wonder that this emotional hangover still lingers. Valentine’s Day is a perfect time to reject the idea that the ideal man is taller, richer, more knowledgeable, more renowned or more powerful. The most important predictor of marital happiness for a woman is not how much she looks up to her husband but how sensitive he is to her emotional cues and how willing he is to share the housework and child-care. And those traits are often easier to find in a low-key guy than a powerhouse.
I am not arguing that women ought to “settle.” I am arguing that we can now expect more of a mate than we could when we depended on men for our financial security, social status and sense of accomplishment. But that requires ditching the Lois Lane syndrome, where we ignore the attractions and attention of Clark Kent because we’re so eager for the occasional fly-by from Superman.”

Friday, 27 May 2016

JPM: Wazee wameharibu nchi

Imechapishwa gazeti la Mtanzania: Fri, May 27th, 2016


RAIS Dk. John Magufuli*Asema atabanana na wala rushwa kila kona
*Aeleza yuko tayari kuchunga ng’ombe kijiji
NA ESTHER MNYIKA, DAR ES SALAAM
RAIS Dk. John Magufuli  amesema wazee ndiyo wameharibu nchi hadi ilipofika sasa.
Amesema yuko tayari kurudi kijijini kwao akachunge ng’ombe kuliko kuwavumilia wala rushwa   nchini.
“Wazee tukitoka tuacha nchi safi, sisi wazee  ndiyo tumeharibu nchi hapa tulipofikia,”alisema Rais Dk. Magufuli
Rais alisema kutokana na uozo uliojaa serikalini, lazima ataendelea kuwachukulia hatua wanaokiuka taratibu za utumishi hadi   watendaji watakapobadilika.
Aliyasema hayo     alipofungua  mkutano wa Bodi ya Wakandarasi Tanzania, Dar es Salaam jana.
Alisema watendaji wa Serikali yake ni lazima wabadilike akisisitiza kuwa suala la utumbuaji majipu kwake siyo la muda mfupi na hatalibadili kamwe.
Kiongozi huyo wa nchi, alisema atahakikisha anaongeza vijana wengi katika  Serikali yake kwa sababu  hawapendi rushwa ingawa kuna watu wamekuwa wakiwachukia.
Alisema   atahakikisha   anajenga nidhamu ndani ya Serikali kwa kuwa na watumishi wenye kujituma kwa maslahi ya nchi na watu wake.
“Kazi hii  nilipewa na Mungu  sikupewa na mtu  yeyote, nipo  tayari kutoa sadaka mwili wangu kwa ajili ya watanzania wanyonge.
“Huo ndiyo mwongozo katika utendaji wangu  kamwe sitabadilisha, nitawashughulikia kweli kweli,” alisema Rais Magufuli.
Akizungumzia changamoto ndani ya Serikali, alisema  pamoja na hali hiyo bado anafahamu umuhimu wa sekta ya ujenzi katika maendeleo.
Rais alisema serikali yake ipo tayari kuwapa kipaumbele wakandarasi wa Tanzania   inapotangazwa zabuni za miradi ya ujenzi.
Lakini amewataka kujirekebisha kwa kupanga viwango vinavyostahili vya gharama za ujenzi wa miradi hiyo ambavyo serikali itaridhika.
“Nawatolea mfano… idara ya mahakama imetangaza kujenga mahakama za mwanzo na za wilaya, kwenye bajeti wana Sh bilioni 24.
“Makadirio ya kitaalamu yanaonyesha kila jengo lisizidi Sh milioni 200, wakandarasi wazalendo walipoomba katika nyaraka zao wametaka jengo moja lijengwe kwa Sh bilioni moja  na Sh milioni 400!
“Sasa nakuuliza Mheshimiwa Mwenyekiti na ndugu wakandarasi, hata kama una upendeleo, upendeleo huo utapasua moyo. Hata kama utakuwa na upendeleo kiasi gani kwa wazalendo utashindwa.
“Sasa mimi niwaombe ndugu zangu wakandarasi, pamoja na nia nzuri ya serikali kuwasaidia wakandarasi wazalendo, ni lazima na ninyi muwe na nia nzuri ya kuisadia nchi,” alisema.
Rais aliwataka wakandarasi hao kuacha kutoa rushwa kwa watendaji wa serikali   wanapoomba zabuni za ujenzi na badala yake watoe taarifa kwa Taasisi ya Kuzuia na Kupamba na Rushwa (Takukuru)    watendaji hao wakamatwe na kuchukuliwa hatua za  sheria.
“Mimi niwaombe wakandarasi, msikubali kutoa rushwa, na muwafichue watendaji wanaoomba rushwa.
“Atakapokuomba wewe rushwa hujui amewaomba wangapi, na utakapotoa rushwa huna hakika kama ile tenda utaipata.
“Wengine wameishia kutoa rushwa hapa, rushwa hapa, rushwa hapa, mpaka anafilisika… kazi huipati na rushwa umeitoa,” alisema.
Vilevile, amewataka wakandarasi hao kujipanga ipasavyo  waweze kupata zabuni katika kutekeleza miradi mikubwa ya ujenzi   nchini ikiwamo ujenzi wa bomba la mafuta  kutoka Hoima  Uganda hadi bandari ya Tanga, ujenzi wa Reli ya Kati na ujenzi wa viwanda.
“Sina uhakika  mmejipangaje wakandarasi wa Tanzania katika kuhakikisha hiyo kazi mnaipata, ya kujenga bomba kutoka Hoima,   Uganda hadi Tanga.
“Nitasikitika sana kilometa zote 1,410 pasiwepo mkandarasi hata mmoja wa kutoka Tanzania.
“Wenzetu wanajipanga, na ninavyoona wakandarasi wa Tanzania wameendelea sana, lakini nashindwa kuelewa kuna tatizo gani linatufanya kutojua changamoto zinazotukabili.
“Tumejipanga kujenga reli ya kati ya Standard Gauge kwenye bajeti ya mwaka huu tunaanza na kilometa 100.
“… lakini kuna fedha nyingine zitatolewa na serikali ya China, tutajenga zaidi ya kilometa 1,200 Standard Gauge, Central Corridor itakayounganisha Mwanza, Kigoma, Burundi na Rwanda. Wakandarasi wa Tanzania mmejipangaje?” alisema na kuhoji Rais Magufuli.
Alisema kwa sasa   sekta ya kilimo  ambayo karibu ya watanzania asilimia 80 wanaitegemea huwezi ukawaacha wakandarasi  kwa sababu dhana wanazotumia  wengi  kwenye kilimo zimetengenezwa na wakandarasi.
Rais Dk. Magufuli alisema kuna sekta  nyingi zinategemea wakandarasi ikiwamo sekta ya uvuvi ambayo imekuwa ikichangia pato dogo kwa Taifa.
Alisema sekta ya madini  ambayo Tanzania imebahatika  kuwa na madini mengi,  karibu madini yote  yanayopatikana duniani,  na Tanzania yapo kwa asilimia kubwa.
“Madini hayo ambayo ni Tanzanite, Diamond Uranium na gram fight hadi gesi ambako tuna quebic feet  zaidi ya trilioni 59 za ujazo, kwa sasa zipo Tanzania.
“Vitu hivyo vinagusa wakandarasi  ukizungumzia suala la miundombinu  kwa sasa   kutakuwa na miradi  mikubwa katika nchi hii,”alisema Rais Dk.Magufuli.
Alisema imepangwa bajeti karibu asilimia 40 ambayo zaidi ya  trilioni 10 zitakwenda  kwenye miradi ya maendeleo na asilimia 46 zitakwenda  kwenye Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasilano.
RUSHWA
Rais Dk.Magufuli alisema   miradi hiyo inaweza kumalizika kwa  Sh milioni 200 ‘lakini unajua kabla hujamaliza lazima upeleke asilimia kwa mtu fulani’.
“Hiyo inaweza kuwa ni sababu  na kama hiyo ni sababu tuna chombo chetu, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na kwa nini hamkitumii?  Kwa nini mnaungana na wale wanaomba rushwa?” alisema.
Alisema  kila mahali wanapokwenda kuomba zabuni wanaweka maslahi ya asilimia kwa ajili ya  kuchukua rushwa.
“Nimemleta hapa  Mkurugenzi wa Takukuru japo hakualikwa  kwa sababu ni mtu ninayemwamini.
“Inawezekana mnaowapelekea kesi nao ni wala rushwa. Huyu namwamini, kama kuna tatizo la rushwa  peleka taarifa   kwa Valentino,” alisema.
Akizungumzia madeni kwa wakandarasi, alisema  pamoja na kuwapo   tatizo la kuyalipa, Serikali itahakikisha inayalipa kwa wakati.
Kama ni tatizo la kulipa madeni yao sasa  limekwisha  na   Waziri wa Ujenzi, Uchuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, amekwisha kulipa Sh bilioni 650, alisema.
Makombora
Rais Dk.Magufuli alisema changamoto kwa  wakandarasi  ni kutokuwa na ushirikiano na ubinafsi  ambao  ni ugonjwa  unaotakiwa kuombewa.
Alisema changamoto nyingine ni  wakandarasi  kutumia majina ambayo siyo yao.

Huu Udhalilishaji wa huyu Harmonizer Kusema Sepetu Katoa Mimba inaweza kumpeleka Jela Harmonize

WEMA2Wema Isaac Sepetu ‘Madam’

Dar es Salaam: Endapo mkali wa sinema za Kibongo, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ atalivalia njuga suala la kudhalilishwa mtandaoni na msanii aliye chini ya Lebo ya Wasafi Classic Baby (WCB), Rajab Abdulhan ‘Harmonize’, jamaa huyo atakwenda jela miaka kadhaa na faini juu.
harmonize kasuku - bekaboyRajab Abdulhan ‘Harmonize’
CHANZO NI NINI?
Juzikati, Harmonize au Hamo, akiwa na kundi la wasanii wenzake katika eneo ambalo halikujulikana ni wapi, walijichukua clip (kipande cha video) kwa staili ya kujipiga ‘selfie’ huku Harmonize akiimba wimbo wa msanii Stamina uitwao Mwambie Mwenzio, ambao kwenye mistari hiyo dogo huyo alisherehesha kwa kusema kuwa, usitoe mimba usije ukaja kulia kama (Wema) Sepetu.
HARMONIZE ALA ZA USO
Baada ya Harmonize kuwaongoza vijana hao kumdhalilisha Wema kwa staili hiyo, watu wengi kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii walimpa jamaa huyo za uso, baadhi wakisema kuwa, umaarufu mdogo alioupata unamzuzua.
Wema SepetuWema na mama yake mzazi.
“Huyu mtoto anaona ameshakuwa maarufu sasa, anaona sawa kuwatukana hata wakubwa zake au ametumwa?” alihoji mmoja wa mashabiki wa Wema (Team Wema) aliyejitambulisha kwa jina la C_K kwenye Mtandao wa Instagram.
Mwingine akaandika: “Ninachojua huyu dogo anatafuta kiki lakini siyo kwa kufanya mambo haya, hivi ana ushahidi gani kama Wema katoa mimba?”
Harmonizer-na-WolperHarmonize na Wolper
KAULI YA TCRA
Akizungumzia sakata hilo, Afisa kutoka Dawati la Malalamiko wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Doris Mhimbira alisema kuwa ni kosa la jinai ambalo mlalamikaji akiwa ‘serious’ anaweza kusababisha Harmonize akachukuliwa hatua kali za kisheria.
Alisema kitendo alichokifanya Harmonize, endapo Wema atakwenda kulalamika na uzuri ni kwamba jina la mlalamikiwa linajulikana hivyo sheria itachukua mkondo wake. (Kwa mujibu wa sheria ya mtandao anaweza kwenda jela kati ya mwaka mmoja hadi saba na faini juu.)
Hata hivyo, taarifa zilizopatikana ni kwamba Wema hajalikalia kimya suala hilo kwani anadaiwa kawasiliana na wanasheria wake ili kumfunga jamaa huyo.
MAMA WEMA SASA
Hata hivyo, wakati kila kona yakirushwa makombora kuelekezwa kwa Harmonize na timu yake (Team Harmonize), yakavuja madai kuwa, mama wa Wema, Mariam Sepetu aliona clip hiyo na kwamba alikwenda kwenye Kituo cha Polisi cha Kijitonyama (Mabatini) ili kushinikiza kijana huyo kukamatwa na sheria ichukue mkondo wake.
WEMA AJIBU KIAINA
Baada ya Wema kuona clip hiyo alionekana kuumizwa na maneno hayo, akaamua kutupia picha mtandaoni akiwa na mama yake kisha akaandika; ‘Ipo siku na mimi nitaitwa mama’.
HARMONIZE ATAFUTWA!
Kufuatia ishu hiyo kuwa gumzo mjini huku kila mmoja akimlaumu Harmonize, Ijumaa lilimtafuta kupitia simu yake ya mkononi ambapo alipopatikana alisema, anashangaa watu kumjia juu kwa kuwa yeye hakumtaja Wema kwenye clip hiyo ila jina lililotajwa ni Sepetu.
“Tuachane na hayo mambo bwana, mimi sijamtaja Wema pale, jina lililotajwa ni Sepetu sasa Wema na Sepetu wapi na wapi?” alijitetea Harmonize.
SEPETU GANI?
Alipobanwa kuwa ni Sepetu gani ambaye walikuwa wakimlenga ambaye ametoa mimba, hakujibu badala yake alikata mawasiliano.
IJUMAA LAMTAFUTA MAMA WEMA
Mwandishi wetu alifanya jitihada za kumtafuta mama Wema ili kujua aliichukuliaje clip hiyo na kama ni kweli alikwenda polisi, hata hivyo simu yake iliita kwa muda mrefu bila kupokelewa.
WEMA HUYU HAPA
Baada ya mama Wema kukosekana, Ijumaa lilipata fursa ya kuwasiliana na Wema ambaye katika hali ya kuonesha kutofurahishwa na kitendo hicho, alimbutua Harmonize kwa kusema kuwa hajitambui ndiyo maana anafanya mambo ya kitoto.
“Kwanza nipo bize sana na kazi, hao ni watoto wadogo hao hawajielewi,” alisema Wema.
Alipoulizwa kwamba huenda ni mpango wa kumtibulia mchongo wake anaoupigia kampeni wa Wema App, mwanadada huyo alisema kama ni hivyo yeye na walio nyuma yake siyo wasomi na bora kuachana nao.
Hata hivyo, taarifa zilizovunjwa ni kwamba, Harmonize anafanya kila awezalo ili kumpa mimba mpenzi wake wa sasa, mwigizaji Jacqueline Wolper Massawe.
Harmonize alipoulizwa kuhusu hilo alisema kuwa, hiyo ni mipango ya Mungu na ikitokea itakuwa mwake tu.
TUJIKUMBUSHE
Katika mambo ambayo yamekuwa yakimuumiza Wema ni pamoja na watu kumuita mgumba sambamba na kumpa skendo ya kutoa mimba kila anaponasa.
Katika siku za hivi karibuni, Wema alinasa mimba lakini inavyonekana haikuwa riziki kwani miezi kadhaa baadaye ilidaiwa kuchopoka.

KAMA MZAZI: Uko wapi mwarobaini wa mmomonyoko wa maadili?



TANGU zama za kale wahenga walikuwa na misemo yao iliyotumika kutoa onyo na mafunzo mbalimbali kwa jamii. Misemo hiyo ipo ya zamani bila kusahau inayoibuka siku hizi ikiwa na nafasi muhimu katika jamii.
Mmoja wa semi hizo ni ule unaosema ‘Mwenzako akinyolewa, wewe tia maji.’ Maana kubwa ya usemi hii ni kwamba kama unashuhudia mwenzio ananyolewa ni vizuri wewe ambaye uko katika foleni ya kusubiri kunyolewa, utie maji, hatua itakayozifanya nywele zako ziwe laini ili wakati wako ukifika wa kunyolewa hatua hiyo iwe imeshafanyika kiasi kwamba hutosikia mikwaruzo au maumivu kama mwenzio ambaye alinyolewa bila kutia kwanza maji.

Kona hii ya Kama Mzazi, hapo inafahamu kwamba ni vizuri mtu akajiandaa mapema kama ana mpango fulani anaotaka kuutekeleza ili wakati ukiwadia kwa ajili ya utekelezaji wake asipate vikwazo.
Matukio ya ukosefu wa maadili yanazidi kuongezeka siku hadi siku katika jamii yetu kiasi cha kutoa ishara kwamba Watanzania wameanza kuzoea na kuona kuwa ni jambo la kawaida katika maisha yao ya kila siku.
Hali hii si njema kwani inaweza ikapindukia kuwa utamaduni na vizazi vikaanza kurithishana. Siku hizi kila kukicha hukosi kusikia katika vyombo vya habari vitendo vya ubakaji, ulawiti, ukatili wa kijinsia au ngono zembe tena si kwa watu wazima tu bali hata wanafunzi wa shule za msingi na sekondari.
Yapo matukio ya wanafunzi kushiriki ngono na akinadada poa kwa malipo ya Sh 2,000, yapo matukio ya ndoa za utotoni, kuacha shule kwa kupata ujauzito na hata walimu wa shule za msingi, sekondari na hata vyuo vikuu kufanya mapenzi na wanafunzi wao ambao kimsingi wao ni walezi wao, sawa na wazazi wao.
Katika tasnia ya habari tunaweza kusema hizi ni habari zinazopamba habari za kijamii katika taifa letu kila kukicha kama vile tunafanya kampeni dhidi ya ugonjwa wa Ukimwi au malaria. Hivi kama hali ikiendelea hivi kwa miaka mingine 10 ijayo, Tanzania yetu itakuwa ni jamii ya aina gani?
Mmomonyoko huu mkubwa wa maadili unaotukabili na kujichimbia kwenye jamii yetu tutaudhibiti vipi? Wataalamu wa masuala ya kisaikolojia, afya na kijamii mko wapi? Narudia usemi wetu wa awali kwamba Ukiona mwenzako ananyolewa, wewe tia maji.
Hapa Kama Mzazi inamaanisha kwamba mmomonyoko huu utamgusa kila mmoja kwa nafasi yake kama mzazi, mlezi, mwalimu au mwananchi tu wa kawaida. Wakati umefika sasa wa wataalamu wetu waliobobea katika sekta na nyanja mbalimbali kuketi kwa pamoja na kufanya utafiti na uchambuzi wa jinsi ya kuweza kukabiliana na kadhia hii kwa muda mfupi na pia kwa muda mrefu kama jamii kwa lengo la kurejesha ustawi na ustaarabu wa jamii yetu.
Hakuna kinachoshindikana kama nia thabiti ya kukabiliana na tatizo hili itakuwepo. Wataalamu wakishapata kiini na namna ya kukwamua basi bila shaka serikali, wananchi na wataalamu kwa ujumla wao washikamane na kuingia vitani dhidi ya mmomonyoko wa maadili katika jamii yetu.
Umoja ni nguvu na katika hili tusifanya mzaha. Tuliwekee mikakati ya uhakika na uhalisia itakayotutoa katika kadhia hii ambayo kwa bahati mbaya bado hatujapata njia bora na ya kudumu ya kukabiliana na tatizo hili.
Jambo moja la kutufariji ni kwamba kila mmoja wetu sasa analiona na kulishuhudia hili na kwamba hakuna ubishi kwamba tuna tatizo. Kujua tatizo ni hatua moja mbele ya kutaka kulitafutia ufumbuzi. Tushikamane tujinasue.

JPM kaepusha ‘vita’- Makinda


SPIKA mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Tanzania, Anne Makinda amesema kuchaguliwa kwa Dk John Magufuli kuwa Rais wa Awamu ya Tano, kumenusuru Watanzania na machafuko yaliyokuwa yakielekea kutokea.
Huku akipongeza mtindo wa Magufuli kuweka nchi sawa maarufu utumbuaji majipu, ambao umekuwa ukikosolewa na viongozi wa Chadema, Makinda amesema machafuko hayo, yalikuwa yasababishwe na tofauti kubwa ya vipato vya wananchi baina ya masikini na matajiri.
Alisema hayo jana alipozungumza na wanahabari k
wenye mkutano wa kupitia utekelezaji wa Programu ya Kuendeleza Kilimo Kusini mwa Tanzania (Sagcot), katika Kongani ya Ihemi inayohusisha mikoa ya Iringa na Njombe.
“Tungeendelea tulivyokuwa tunaendelea, hakika tungekuja kuuana kwa sababu wenye nacho waliendelea kupata zaidi na wasio nacho waliongezeka kwa kuwa watumwa wa wenye nacho,” alisema Makinda.
Kauli hiyo ya Makinda, imekuja wakati viongozi wa Chadema wakionekana waziwazi kutetea watuhumiwa wa matumizi mabaya ya madaraka na ubadhirifu wa mali za umma ambao wamekuwa wakichukuliwa hatua na uongozi wa Rais Magufuli.
Utetezi huo ulianza kutolewa na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe mwanzoni mwa Februari mwaka huu, ambapo wakati huo alionya alichoita fukuza fukuza ya watumishi wa umma bila utaratibu, huku akiomba viongozi wa dini kumsaidia kukemea.
Baadaye alikuja kuungwa mkono na makada wa chama hicho, akiwemo aliyekuwa mgombea wa Urais kupitia Ukawa, Edward Lowassa na mwanasheria wa Chadema, Tundu Lissu, ambaye mbali na kuwatetea watuhumiwa hao, alishauri watuhumiwa hao kwenda mahakamani akidai Rais Magufuli anaongoza nchi kama mali yake binafsi.
Mamilionea bila kazi
Makinda katika mazungumzo yake ya jana, alisema bahati mbaya iliyokuwa ikilikumba Taifa ambayo mwenye suluhisho lake ni Rais Magufuli, ni baadhi ya matajiri kutoeleweka wanafanya kazi gani, lakini wakifikia mafanikio waliyonayo kutokana na kunufaika kijanjajanja na fedha za Serikali.
“Kuna watu walikuwa hawaeleweki wanafanya kazi gani, lakini ni mamilionea, baadhi yao ndio wale walikuwa wananufaika na mamilioni ya Serikali,” alisema.
Makinda alisema katika kuiweka nchi sawa katika nyanja mbalimbali, kila Mtanzania ataonja machungu yatakayokuja kuliponyesha Taifa mbele ya safari.
“Kutakuwa na magumu, wengi watasema aah huyo bwana mbona kabana hivi, lakini ni muhimu Watanzania wajue hii ni oparesheni kubwa itakayotuumiza wote, lakini mwisho wa yote Taifa na Watanzania tutapona,” alisema.
Aliwataka Watanzania waendelee kumuombea kwa Mungu Dk Magufuli ili aendelee kuwa na afya njema, busara na afanye kazi kwa kasi aliyoanza nayo hadi atakapomaliza awamu yake.
Wanaompinga
Wakati Makinda akitoa kauli hiyo, Mwenyekiti wa Chadema Mbowe baada ya kukosa kuungwa mkono na viongozi wa dini aliomba wamkemee Rais Magufuli mwanzoni mwa Februari, alikuja kuungwa mkono na Lowassa.
Lowassa yeye alidai kuwa utumbuaji majipu umesababisha hali mbaya ya maisha kwa wananchi, kwa kuwa watumishi hao wa umma wameachishwa kazi. Mgombea huyo alienda mbali zaidi na kudai kuwa, anasononeshwa anapoona watu wanaachishwa kazi katika mashirika ya umma.
Mbali na Lowassa, Lissu ambaye mbali na kuwa mwanasheria wa Chadema, pia ni Waziri Kivuli wa Katiba, mwanzoni mwa mwezi huu, alidai bungeni kuwa Rais Magufuli amesababisha hofu ya kutumbua majipu kutanda nchi nzima, huku akimtuhumu kuwa ana viashiria vya udikteta.
Wanaomuombea
Wakati Makinda akiomba Watanzania wamuombee Rais Magufuli, huku viongozi wa Chadema wakipambana na hatua anazochukua dhidi ya wabadhirifu wa mali za umma, Askofu Mkuu wa Kanisa la Assemblies of God (TAG), jimbo la Kilimanjaro, Glorious Shoo, amesema uongozi wa Rais Magufuli, ni majibu ya maombi ya Kanisa na matarajio sahihi waliokuwa nayo Watanzania wote.
Askofu Shoo aliyasema hayo jana wakati akizungumza na gazeti hili ofisini kwake, ambapo alisema kwa sasa heshima ya nchi imerudi baada ya mataifa mengine ya nje kujionea uongozi wa Rais Magufuli unavyopiga vita rushwa na dawa za kulevya.
Alisema kwa sasa Rais Magufuli, ameweza kurudisha ramani ya Tanzania iliyowekwa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, na kueleza kasi ya utumbuaji majipu inayoendelea ni jambo la kumshukuru Mungu, kwa kuipatia nchi kiongozi anayethubutu kuchukua hatua, bila woga kwa ajili ya kusaidia wanyonge.
Askofu Shoo alisema atashangazwa kuona kiongozi yeyote wa kisiasa atakayepinga yanayofanywa na Rais, kutokana na uwajibikaji na nidhamu mahala pa kazi kurudi.
Alipongeza hatua alizoita za kuponya fedha kwa kuwawajibisha watu waliosababisha upotevu wa fedha na kufanya mabadiliko yaliyochangia kuokolewa kwa fedha za umma, hali iliyosababisha heshima ya nchi kurudi katika mataifa mengine.
“Utendaji kazi na aina ya uongozi wa Rais Magufuli ni majibu ya maombi yetu sisi Kanisa na tunamuunga mkono kwa asilimia zote, kwani yale masuala makubwa na ya msingi ameyafanyia kazi bila woga wowote, ikiwepo vita dhidi ya rushwa, matumizi na biashara ya dawa za kulevya, uwajibikaji na nidhamu mahala pakazi, ni moja ya baadhi ya maeneo aliyoyagusa kwa muda mfupi na kuonesha matunda yake.
“Ukisafiri sasa sehemu mbalimbali za dunia, wanakueleza wanafahamu habari za Tanzania kama moja ya nchi inayopambana na rushwa kwa kasi kubwa pamoja na biashara ya dawa za kulevya, ambapo hapo awali Tanzania ilitajwa zaidi kwenye masuala ya kupitisha dawa za kulevya, lakini kwa kipindi hiki cha uongozi wa Awamu ya Tano hali imekuwa nzuri,” alisema Askofu Shoo.
Upinzani usipuuzwe
Alishauri viongozi wa upinzani wasipuuzwe licha ya baadhi yao kuwa na tabia ya kupinga vitu vinavyofanywa na Serikali, ambapo aliitaka Serikali kuchuja masuala ya msingi yanayosemwa na viongozi hao, ili yanayoweza kufanyiwa kazi kwa manufaa ya Watanzania wote katika kuiponya nchi, yafanyiwe kazi.
Alisema sasa ni muda wa kuweka siasa pembeni kwa vyama vyote, ili vishirikiane na Serikali iliyopo madarakani, ili mambo ya kweli yanayopigiwa kelele na upinzani kama yana ukweli yafanyiwe kazi na wananchi waridhike kweli yamefanyiwa kazi.
“Siasa ikae pembeni tuiponye nchi yetu wapinzani na Serikali kwa kumuunga mkono Rais Magufuli ...lakini tutaogopa kama kila jambo linalotoka kwa wapinzani litatupwa, tunatarajia baadhi yatafanyiwa kazi, pia wapinzani nao tutawashangaa sana wakipinga kila kinachofanyika na Serikali ya Awamu ya Tano,” alisema Askofu Shoo.
Alisema kwa sasa ni vyema Rais Magufuli aweke mfumo sahihi utakaokwenda na kasi yake, ili viongozi wengine watakaokuwa kwenye nafasi mbalimbali, wasitoke nje ya mfumo huo, ambao utazuia matatizo yasitokee.
Imeandikwa na Frank Leonard, Njombe na Arnold Swai,Hai.

‘Wafugaji wasipodhibitiwa watachunga hadi Ikulu’


Mbunge wa Nkasi Kaskazini, Ally Kessy.   MBUNGE wa Nkasi Kaskazini, Ally Mohamed Keissy (CCM) amesema kama wafugaji wataachwa waendelee kuzurura ovyo nchini, ipo siku watachunga ng’ombe hadi Ikulu. Aidha, wabunge jana na juzi wameungana na kueleza kuwa siyo sahihi kwao kuendelea kunyoosheana vidole kati yao kuhusu migongano ya wakulima na wafugaji badala yake serikali ije na mkakati wa kupanga matumizi bora ya ardhi, kwani wote wanahitajika.
Akichangia hotuba ya Waziri wa Maliasili na Utalii juzi bungeni, Keissy alisema si sahihi kuwaacha wafugaji waendelee kuchunga kila eneo nchini bila kuwa na udhibiti maalumu. “Tunasema asilimia 75 ya Watanzania ni wakulima, kwa hiyo kama wengi ni wakulima, sasa kama ni kumjali basi tumjali mkulima kwani mvua zikikosekana kwa kuharibu mazingira, hatuna uwezo wa kilimo cha umwagiliaji”.
Hatuwezi kuendelea kutishana humu ndani. Lazima wafugaji wafuge kwa kufuata taratibu. Tukiwaachia hawa ipo siku wafugaji watachunga ng’ombe hadi Ikulu,” alisema Keissy.
Akizungumzia ujangili, mbunge huyo matata alisema ni vyema askari wanyamapori akikuta mtu ameingia katika hifadhi bila ruhusa, ampige risasi kwa sababu akimwacha anauawa yeye (askari).
Kwa upande wake, Mbunge wa Muhambwe, Atashata Nditiye (CCM), alisema lazima wabunge waache siasa na kuweka mbele maslahi ya Taifa vinginevyo nchi itageuka jangwa.
Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa (Chadema) alisema badala ya kugombana, lazima maslahi ya Taifa yawekwe mbele na kuwapo na mipango madhubuti ya kutenga maeneo ya wakulima, wafugaji, samaki na shughuli nyingine za kiuchumi.

Thursday, 26 May 2016

African Cultures - Good Cultures and Bad Cultures

Africa, as in other parts of the world, there are many traditions 

which the fore-fathers instituted.  Some of these traditions 
are good in that they tend to guide the people to 
maintain law and order in the communities.
 

Some are actually bad and are being rejected, especially by the civilised society, the Islamic and Christian societies. These bad beliefs and practices were instituted in the olden days, mainly due to ignorance and superstition but are still practiced today in some communities with strong enforcement. 


Ill-Treatment of Widows.....
Areas of bad cultures, in Africa, which affect women most are where widows are made to shave their head and move about in complete black clothing everywhere they go for one year. This is a compulsory act of respect for the dead husband which the widow must carry out whether she likes it or not. In fact this is practised in almost every community in Africa, the civilised groups are making effort to modify it so that the widow may not shave her head but should mourn the dead husband in black clothing, and some places white clothing for only six months. But this modification is rejected in many communities where they demand full observation of the mourning right.


Widows To Drink Water Used To Wash Dead Husband…..
 In some communities widows are subjected to some wicked belief where they are told to drink the water used to wash the dead husband’s body. The reason given for this is to show that she is innocent of the husband’s death. If she did not die within certain number of days after drinking the water, that will exonerate her from killing her husband. Of ‘curse, this act is being kicked against by the religious groups but is still practised in many communities with strong enforcement. Any refusal by the widow to carry out this part of the culture is met with grievous punishment, including madness. 


 
Killing of Twins……
 A little child is not only precious to behold, but also one among the beauties nature bestows on mankind; a child is therefore a wondrous creature and as such ought to have some dignity attached to his or her personality. Among the Yoruba people of Nigeria, twins are called ibejis after Ibeji. People believe that, depending on how they are treated, twins can bring either fortune or misfortune to their families and communities. For this reason, twins receive special attention. Also, in some parts of the Ivory Coast, twins are also said to be able to stop the rain and are often called upon when there are manifestations or events and the weather turns inclement. In Guinea and in the Ivory Coast, when one twin is getting married, the other is also treated like the bride.

Unfortunately, not all communities share favourable superstitious belief about twins. Some communities believe those twins, or any birth exceeding one at a time is an abomination and that the twins should be killed as soon as possible. In most cases a sacrifice should be carried out by the family to appease the gods. It might surprise you that this horrible and wicked practise still exist today in many parts of Africa with strong enforcement. I remember where I used to work in south southern part of Nigeria. A young man was telling us that it should not be heard or spoken that a twin is born in their place. I told him that I love twins but he told me not to speak it outside because it is abomination. I was surprised, but he was defending the practice with strong confidence, even boasting about it….I wondered, how can culture be this wicked? 

In the Calabar region of Nigeria, killing of twins was practiced strongly but the good old Mary Mitchell Slessor, a Scottish Missionary to [Calabar] Nigeria, fought strongly against it bringing the practise to a stop. When she started the fight against the killing of twins, people called her names, regarding her as eccentric but she determined and brought the killing to a stop.


First Daughters – Not Allowed to Marry….
In some parts of Africa, first daughters are not allowed to marry They are to stay in the family to reproduce in other to perpetuate the family name. This is mostly practised by the Ikwere, Ogoni, etc. tribes of Nigeria. Even as the Christian groups are fighting against this practise, the traditionalists still strongly enforce it. 


 …..Just take a simple instance of where a young girl finds a handsome man of her choice that she wants to take as her husband. The parents say she must not marry the man because the custom is that she must not marry [as she is the first daughter who must not marry]. She refuses, and she is castigated, even cursed with madness…..

The above mentioned are some examples of bad cultures [More in later posts] which were ignorantly instituted in the olden days by the fore-fathers. Not only that these cultures are bad, but that some wicked and evil men trickily hide under its guise to oppress the weak. 
I am not writing this to make it look like Africa is so bad a continent or her countries so bad a place to live. But we should look into the bad cultures and make effort to stop them. These bad cultures not only cause grief and sadness to the people, but they also portray Africa as a primitive, if not wicked type of race. 


Take the case of castigating a healthy, energetic person to madness. This act is so shrouded in secrecy by the traditionalists. False stories are told about the poor fellow so that people will treat him/her as mad, ill-treating him, even using all sort of witchcraft on him. Eventually the poor fellow falls sick or loses control of self. Why should we have cultures that bring unhappiness to the people or maintain cultures that allow people to use for wickedness?

SMGEO is here to educate the society about bad beliefs
Join with us
smgeo2015@gmail.com