Tuesday 10 May 2016

NYIE WABABA "MSIWANYANYASE WATOTO WA KAMBO" TIMIZENI AHADI ZENU KAMA MLIVYOWAAHIDI MAMA ZAO KABLA YA KUWAOA KUWA MTAWATUNZA!!

na Veronica Sheiza,
Tunapozungumzia suala la mtoto .tunamlenga baba na mama.

Inanisikitisha sana kuona baba anaoa mama ambae anamtoto wa baba mwingine.wanawaita watoto wa kambo.

Yule baba anamuahidi mama "nitakutunza pamoja na mwanao".


Baada ya muda fulani wa miaka kadhaa wanapata watoto .Hapo baba anaanza visa kwa yule mtoto amesahau ahadi zake kwa yule mama.

Kibaya zaidi sana ukute yule mama aliolewa hana kazi; sasa baada ya muda yule 

baba  anaanza kumnyanyasa yule mtoto tena kwa ukatili mbaya na mama 

anapoingilia  anapigwa pamoja na mwanae .

Hapo ndo nashindwa kuwaelewa kama 

hawajui kwani watoto ni  Taifa la kesho.na 

mtoto wa mwenzio ni wako .

Akina Baba badilikeni,suala la kunyanyasa  watoto kwa kigezo sio wa kwako ni kosa 

kubwa. Kumbuka mtoto wa mwenzako ni  mwenzako.

Veronica Sheiza- Muuguzi na mtaalam wa 

masuala ya mahusiano na saikolojia

HEBU TUKOMESHE MIMBA ZA UTOTONI KWA WATOTO WALIOPO SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI TANZANIA

Mtoto ni rasilimali ya leo kesho na keshokutwa. 
Kitendo cha kuwanyamazia wale wanaowatongoza au kuwarubuni watoto hawa ikiwepo mabinti wa shule za sekondari mijini na vijijini ni kosa kubwa sana tunalolifanya sisi kama wanajamii.
Suala la kuwakemea hawa wachafuzi wa watoto wetu wanaosoma nijukumu la kila mtoto,kijana,mtu wa makamo na  mzee   yeyote yule kuwalinda watoto hawa wasiharibiwe malengo yao na watu wachache wenye mihemuko ya uharibifu.
Maisha mazuri ya watoto wanaosoma hasa wa kike yanategemeana na jinsi ambavyo sisi kama jamii tunawalinda na kuwaheshimu kama watu muhimu kwa jamii yetu.
Hawa ndio wabunge,makatibu marais, mawaziri na wakurugenzi wa kesho lakini ndio maafisa mipango wa kuanzia usiku wa leo na kuendelea.
Tuwathamini watoto wa kike, tuache kuwarubuni , tuwasaidie kutimiza ndoto zao.
kampeni hii imeletwa kwenu na Shirika lisilo la kiserikali na Masuala ya Jinsia.
Social Mainstreaming for Gender Equality Organization
P.O.BOX 6444
Morogoro, Tanzania
Barua pepe: smgeo2015@gmail.com