Monday 23 May 2016

FAHAMU MADHARA MAKUU MATANO YA KULAMBA SEHEMU ZA SIRI (KUZAMA CHUMVINI ).

Kukua kwa kasi ya utandawazi kumeleta maendeleo makubwa ya kijamii, kiuchumi na kisiasa. Pamoja na hayo yote kuna mambo ya ambayo waafrika tumeyaiga nikiimanisha ambayo sio jadi yetu pia ni hatari kiafya hapa nikimaanisha kulambana sehemu za siri kabla ya ngono bila kujua madhara makubwa yasababishwayo na tabia hiyo.


Leo hii kuna watu hawaridhiki na kufanya ngono bila kulamba au kulambwa sehemu hizo za siri lakini leo naomba nikupe madhara makuu ya kushiriki aina hii ya ngono..

Kansa ya koo: kirusi ambacho kinasababisha kansa ya mlango wa uzazi kwa mwanamke huweza kuambukizwa na kushambulia koo la chakula na kusababisha kansa ya koo, ambayo ziku zote husababisha kifo kwani haina matibabu ya kuponya kabisa.

Magonjwa ya zinaa; haya ni kama gonorea, kaswende na herpes simplex ambayo huanza kwa kushambulia mdomo na yamekutwa kwa watu wengi sana ambao hushiriki sana aina hii ya ngono .

Magonjwa ya ini; virusi vinavyosababisha ugonjwa wa ini maarufu kama hepatitis B huweza kuambukizwa kwa njia hii ya kulamba sehemu za siri, huu ni ugonjwa hatari ambao husababisha kansa ya maini mwishoni.

Ugonjwa hatari wa ukimwi: japokua tafiti zinasema sio rahisi kuathirika na ugonjwa wa ukimwi kwa njia ya kulamba sehemu za siri ila uwezekano upo wa kupata ukimwi kwa kupitia maji maji ya ukeni au ya uume na michubuko ya mdomoni ya mlambaji.

Magonjwa ya kinywa; bacteria wengi wanaopatikana kwenye sehemu za siri huweza kushambulia sehemu ya wazi ya jino na kusababisha kuoza kwa jino na maumivu makali sana ya meno

Mwisho; haya ni baadhi ya magonjwa yanayofahamika mpaka sasa hivi yatokanayo na aina hii ya ngono…mengine bado yanafanyiwa utafiti sehemu mbalimbali. Onyo; usijaribu au kuiga mambo usiyoyajua kwani unajihatarishia afya yako wewe na mwenzi wako.

                                             Mawasiliano; 0653095635\0769846183

                                              STAY ALIVE………

                           DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO

No comments:

Post a Comment