Wednesday 2 March 2016

UKEKETAJI BADO NI TATIZO SUGU TANZANIA,LHRC NA MASHIRIKA MENGINE WATOA NENO NZITO !!


Mwanasheria kutoka kituo cha sheria na haki za binadamu LHRC ndugu HAROLD SUNGUSIA akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es salaam juu ya siku ya kupinga ukeketaji duniani
NA EXAUD MTEIIkiwa leo ni siku ya kupinga vitendo vya ukeketaji duniani imeelezwa kuwa bado mapambano dhidi ya ukatili huo hapa nchini kwetu Tanzania yanahitaji nguvu ya ziada kwani bado baadhi ya mikoa imekuwa sugu katika vitendo hivyo ambapo serikali imetakiwa kuchakua hatua mara moja juu ya watu ambao wanahusika katika vitendo hivyo.

Akizungumza na wanahabari leo mwanasheria kutoka kituo cha sheria na haki za binadamu LHRC akiwakilisha mashirika zaidi ya 15 yanayohusika na ukeketaji nchini Tanzania wakili HAROLD SUNGUSIA amesema kuwa mwaka 2014 umeshughudia watoto wengi wakikeketa, pamoja na jitihada za kutokomeza vitendo hivyo ambapo ametolea mfano wilaya ya tarime pekee takribani watoto 1400 walikeketwa na watoto hao ni kutoka katika koo za bukira watoto 212,bukenye watoto 230,iregi watoto 800,pamoja na nyabasi watoto 160,ambapo ni idadi kubwa sana na ikizingatiwa kuwa ni wilaya moja tu.IMELDA URIO ambaye ni mkurugenzi wa uwajibikaji na uwezeshaji kutoka kituo cha sheria na haki za binadamu LHRC akizungumza na wnahabari
Amesema kuwa pamoja na kuwepo kwa sheria zinazolikemea tatizo hilo bado cha kusikitisha ni kuwa mila hii imekuwa ikitekelezwa kwa kasi sana katika maeneo mbalimbali nchini Tanzania katika baadhi ya jamii zetu.

“tunaitaka serikali kwa kupitia jeshi la polisi kusimamia sheria na kuwachuklia hatua za kisheria watu wote watakaobainika kufanya vitendo hivi”amesema SUNGUSIAAmeongea kuwa ukeketaji ni kosa la jinai, na kosa la jinai huwa haliishii yani halina ukomo wa muda hivyo wanatarajia kuwa kama serikali inamaanisha kweli kupinga ukeketaji huo basi iweze kufwatilia huko vijijini na kuwabaini wale wote wanaoshiriki kukeketa watoto na kuwachukulia hatua stahikiMwakilishi kutoka chama cha wanahabari wnawake tanania TAMWA bi GOGFUDA JOLA akizngumzia kuhusu shirika lao linavyoshgulikia tatizo la ukeketaji katika maeneo mbalimbali nchini.Wasaka habari wakiwa wanasikiliza kwa makini Aidha mashirika hayo yanayotetea na kupinga vitendo vya ukeketaji wamewaomba wadau wengine na watanzania kwa ujumla kujiuga kwa pamoja kupinga vitendo hivyo kwani ni vitendo vya kikatiki kwa mtoto wa kike na ni kumnyima haki zake za msingi kama mwanadamu,ikiwa ni pamoja na kutoa elimu zaidi juu ya madhara ya ukatili huo.

Baadhi ya mashirika ambayo leo wameungana kwa pamoja kupinga vitendo hivyo ni TAWLA,TAMWA,DIAC,CCT,WORDVISSION,NAFGEM,AFNET,WOWAP,CDF,WLAC,TGNP MTANDAO,WILDAF,BAKWATA,TGNP pamoja na HOUSE OF PEACE

No comments:

Post a Comment