Sunday 10 April 2016

VIJUE VIKWAZO KATIKA UZAZI WA MPANGO VINAVYO IKABILI JAMII



WANAWAKE wengi nchini wana elimu ya kutosha kuhusu uzazi wa mpango. Wanajua kutokana kwa kuambiwa na rafiki zao, kujifunza kwa wazazi, kliniki na kwa kusoma kutoka vitabuni na mahali pengine.
Wanajifunza kwamba uzazi si kitu cha bahati mbaya. Kinasababishwa.
 Baadhi ya akina mama hawa wanataka kuepuka mimba zisizotarajiwa, wanaona hali mbaya ya uchumi, kipato duni na kazi ngumu ya kulea watoto wengi.
Wanawake wengi wanajifunza aina mbalimbali za kupanga uzazi, mfano za vijiti, vitanzi, sindano, kondomu, vidonge na nyingine za asili za kufuata kalenda ya mwili ama wenzi wao wa kiume ‘kuishia nje’.
 
Ukizungumza na wanawake wengi, wasomi na wasio wasomi, wanasema kila njia ni nzuri kwa mtumiaji maadam ameona inafaa.
 
Kwani njia moja inaweza kumfaa na mwingine isimfae. Hata hivyo, wapo baadhi ya watafiti wanaosema kwamba njia nyingi za uzazi wa mpango mbali na zile za asili zina madhara haya na yale. Katika kampeni
yao ya kupanga uzazi, wanawake wengi wanapambana na vigingi viwili vikubwa.

Kimoja ni uhaba wa wataalamu wa kuelekeza utumiaji wa njia salama za uzazi wa mpango na kuadimika kwa njia hizo za kupanga uzazi. Kutokana na vikwazo hivyo, wanawake wengi wamejikuta ama kulazimika kutumia njia za uzazi ambazo hawazipendi, ama zisizo salama na zenye kuwaletea madhara.

Wengine wamejikuta, wakitumia njia ambazo, wanashindwa kuzifuata na hatimaye wanatumbukia kwenye mimba zisizotarajiwa na kuamua kuzitoa.

Bingwa wa Masuala ya Wanawake katika Hospitali, anasema, wanawake wengi wamekuwa wakishindwa kufuata mpango wa uzazi kutokana na kukosa huduma wanazotaka au kukosa wataalamu wa kuelekeza njia mbalimbali za uzazi wanawake wanaotumia njia za kisasa za uzazi wa mpango wameanza kuongezeka katika kipindi cha miaka miwili iliyopita.
 
Anasema ukizungumza na wanawake, wanakubali kwamba wanatumia njia mbalimbali za kuzuia mimba, kupanga uzazi na kuzuia maradhi kwa lengo la kupata muda wa kutosha kufanya shughuli za ujasiriamali. zahanati nyingi hazitoi huduma zote za kupanga uzazi na kwamba zipo baadhi zinatoa njia moja tu kati ya hizi; sindano, vidonge, vitanzi, vijiti, kondomu na kalenda ya mwili.

Ukienda vijijini/kijijini, kutokana na kukosekana kwa mtaalamu katika zahanati nyingi karibu zinashindwa kuendelea na njia yake ya sindano, watu wengi wanamua kuchukua vidonge tena pasipo maelekezo ya mtaalamu maeneo mengi au watu wengi hawana elimu ya kutosha kuhusu vidonge, wakati mwingine alisahau kutumia vidonge, akajikuta amepata mimba ambayo hakupangilia.
 
Matatizo kama hayo yanawakumba wanawake wengi, japo idadi ya hospitali, vituo vya afya na zahanati ni nyingi nchini, lakini hakuna huduma ya kuaminika ya uzazi wa mpango.
 Takwimu za Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii za 2006 zinaonesha kwamba kulikuwa na hospitali 219, vituo vya afya 481 na zahanati 4,679, ambavyo vingi vina uhaba wa wataalamu wa afya na hasa inayohusu
uzazi. Kumekuwa na matatizo katika hospitali na vituo vingi vya afya na hata zahanati za kupata huduma hizo, kutokana na wanawake wengi kukosa uchaguzi wa aina ya njia wanazoona zinawafaa katika kupanga uzazi.


Wanawake wamekuwa wakifika hospitalini, vituo vya afya au zahanati na kulazimishwa kutumia sindano au kondomu, wakati wao wamezoea vijiti au vidonge.

Binti mmoja nilimuuliza anasema, alipoenda zahanati moja aliambiwa kuwa mtaalamu wa kuweka vijiti amesafiri hivyo asubiri hadi atakaporudi au atumie vidonge.
Kwa kupatikana huduma za vidonge tu, Binti huyo alikuwa na wakati mgumu na hivyo kwa hofu ya kupata ujauzito asiopangilia, akaamua kuanza kutumia vidonge ambavyo haikuwa chaguo lake

No comments:

Post a Comment