Tuesday 8 March 2016

· NINA SABABU YA KUMSIFIA MAMA YANGU KWA NIABA YA WANAWAKE WOOTE DUNIANI JUU YANGU-1 !!!

Eric Samuel thinking about my mother "mamabetty".
A. KABLA YA KUZALIWA MIMI Eric Samuel
Mama aliwahi kunambia kuwa kati ya watoto walomsumbua sana kipindi cha ujauzito basi mimi Nilivunja rekodi,nilimtesa sana ,sasa sijui kwa sababu ndio mtoto wa kwanza wa kiume lakini all in all Mamabetty alisumbuka sana wakati amenibeba tumbo.
B. BAADA YA KUZALIWA(WAKATI NI MTOTO MDOGO CHINI YA MIAKA MITANO)
1. Alinambia nililiwahi kuumwa sana typhoid na malaria wakati ninakama miaka mitano huko kijijini Ikasi Manyoni-Singida ambapo tulikuwa tunaishi huko walipokuwa wanafanya kazi kiasi kwamba sikuongea kwa muda wa wiki mbili nimelala tu ikabidi wanipeleke Dodoma hospitali ya mkoa nikiwa kwenye hali mbaya wodi namba 13 ya watoto. Kufika pale nikawekewa drip za maji kama chumba zaidi ya tatu hali ilikuwa mabaya .
Baada ya muda nikawa nafumbua macho nikawa at least nafumba na kufumbua hali ile iliwapa mashakaka wauguzi ikabidi wamwambie mama chukua dawa hizi utaendelea kumuuguza home. Mama akanibeba na kurudi tena huko kijijini kwenye kituo cha kazi, ambapo usafiri pia ilikuwa shida . Basi akiwa njiani basi lilipoishia akiwa anatembea kwa miguu mimi nikiwa mgongoni siongei wala kulia wala kufanya chochote tangu nitoke hospitali nilipokuwa nimelazwa, jua lilikuwa kali akaona apumzike chini ya mbuyu akawa amenilaza chini nikazinduka nikamuita na kumwambia "mamaa maji,mama maji" hapo nikampa mama matumaini nikapoa kuanzia pale nilipokunywa maji. MAMA NI ZAIDI YA MAMA.
2. Wakati nimtoto wa kubebwa mgongoni siku moja alipokuwa anatoka Saranda anaelekea Londoni kwa miguu huko wilaya ya manyoni aliwahi kupotea njia jioni hivyo alizunguka akiwa amenibeba mimi mgongoni na begi kichwani Mama betty alizunguka kutafuta njia msituni ambao ulikuwa na wanyama wakali kama chui tembo na simba lakini juhudi hizo hazikufanikiwa. Kuona imefika usiku sana saa tatu amekosa la kufanya ikabidi aingie kwa kujipenyeza kwenye usio wa miiba kuingia kwenye shamba la mtu ,akatoa nguo kwenye begi na kutandika chini ,Mama yangu akaomba sala pale akanilaza chini tukalala hadi asubuhi. Mungu alivyomwema sikulia wala kumsumbua wala kudhurika na kitu chochote hadi asubuhi. Ndipo alipotafuta njia na kuipata hadi akafka kijijini na kwaacha watu midomo wazi kuwa amewezaje kupata ujasiri wa kulala msituni na mtoto mdogo sehemu ambayo ni hatari bila kudhurika.
BAADA YA KUKUA KWETU NA FAMILIA YETU.
A. Aslimia kubwa sisi maisha yetu ya utoto tumekulia kwa mama.Pale baba alipohamia Dodoma kikazi watoto watano tulikuwa chini ya uangalizi wa mama. Nikiwa darasa la tatu Baba alihamia Dodoma hivyo sisi tulibaki kwa mama ,na mama alitusimamia mimi na wadogo zangu na dada yetu Hilder mpaka tukamaliza shule ya msingi kwa kipato cha kawaida tunasoma kwa hela za kuuza vitumbua na huku tukilima mazao kama mahidi pamba,alizeti,ufuta namaharagwe hivyo ndivyo vilikuwa vyanzo vyetu vya mapato chini ya usimamizi wa mama.
Ili kuhakikisha mwanae nasoma vizuri Mama alinihamishia mjini ambapo nilimalizia shule ya msingi manyoni pale manyoni mjini ndipo nikajiunga na mwanzi sekondary mwaka 2000 nikiwa naishi kwa Babu mzaa Mama Marehemu Mzee Joseph Kwana .
INAENDELEAAA>>>>>>

No comments:

Post a Comment